Saturday, January 23, 2016

Kamati za Bunge kizaazaa

Kamati za Bunge kizaazaa



Zitto, Heche, Sakaya wazirarua, Mtatiro ahoji watakaochaguliwa PAC kama wataweza kuvaa viatu vya ZZK
*Wabunge CCM wapongeza, mwingine awaponda wapinzani awaita malofa
* Chenge, Aerukamba, Ghasia wapewa uennyekiti wa kamati


Kitendo cha wabunge machachari wa upinzani ambao wanasifika kwa uwezo wa kujenga hoja na kusimamia ukweli wa mambo kutoswa katika Kamati nyeti za Hesabu za Serikali (PAC) na ile ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) na badala yake wakajumuishwa kwenye kamati moja ya Huduma na Maendeleo ya Jamii, kimezidi kuibua mjadala mkubwa ndani na nje ya Bunge.
Kuibuka kwa hali hiyo kunatokana na kile ambacho wengi wamejenga hisia kwamba uongozi wa Bunge umefanya uteuzi huo kwa kushirikiana kwa siri na Serikali ili kupunguza nguvu ya kambi rasmi ya upinzani bungeni.
Wapo ambao wamekwenda mbali na kuutupia lawama uongozi wa Bunge kuwa huenda umechukua uamuzi huo kwa shinikizo la chama tawala cha CCM ambacho kipo katika mkakati maalumu wa kurejesha nguvu yake ya kisiasa kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2020 baada ya kuonja machungu ya uchaguzi wa mwaka 2015.

 

No comments:

Post a Comment

Ads 468x60px

Featured Posts