Hapo
mwamzo Mungu aliziumba mbingu na nchi,kisha akamuumba mtu tena kwa mfano wake
wake,ili atawale na kumiliki.Adamu wa kwanza akawekwa kwenye bustani ya
Eden,mahali palipojaa uwepo wa Mungu lkn pamoja na hayo alitenda dhambi na Mungu akamwekea utaratibu mzuri tu
ili asiangamie.Kizazi cha mwanadamu kiliendelea kukua,hata baadae dhambi
iliendelea kutafuna ulimwengu na Mungu akaamua kushughulikia hili kwa njia ya
gharika.
Mwanzo
11:
Wakati
ule watu walikuwa na lugha moja,na usemi mmoja,watu wote walielewana na umoja
na amani vilitawala.Kwa pamoja kwa kiburi na majivuno ya mwanadamu,wakaafikiana
kujenga mnara mreefu(Babeli),ili wamfikie Mungu,na ndipo Mungu akachukizwa na
kuamua kuwavurugha lugha ili wasielewane tena.Mungu akawasambaratisha katika
maeneo mbalimbali duniani ili wasikae pamoja na kuwa kama walivyokuwa mwanzo.
Kutokea
wakati huo mpaka sasa,ulimwengu uliendelea na kizazi cha mwanadamu kiliendelea kukua,hata kufikia nyakati hizi za
utandawazi.
Utandawazi ni
nini?
-Turning
the world into market economy(Kuurudisha ulimwengu kuwa wa uchumi huria).Kwa
tafsiri hii,neno kuurudisha maana yaka wakati flani chumi za ulimwengu zilikuwa
huru,lkn sasa zimefungwa.
-Kwa
maana hii,maana tu ya neno utandawazi linatuthibitishia kuwa kuna wakati mambo
yalikuwa huru lkn uhuru huo ulikoma,na kwa mawazo yangu,uhuru huu ulikuwapo
kabla ya babeli.
-Kwa
hiyo utandawazi ni mchakato wa kihistoria ulioanza na watu kuhama na kusafiri
maeneo mbalimbali ulimwenguni,hasa kutoka bara letu la Afrika.Kwa kuhama au
kusafiri karibu na hata mbali,wahamiaji,wenyeji na wengine walichukua
mawazo,tamaduni,na hata bidhaa na kuzipeleka maeneo
mengine.Kuigilizana,kuazimana na kuishi maisha ya watu wa jamii tofauti
kukaanza kuonekana katika maisha ya watu.
Kwa
hiyo utandawazi kwa maana hii ni kuunganisha chumi mbalimbali za ulimwengu
mzima kupitia
-biashara
-Mzunguko
wa fedha
-Mbadilishano
wa teknolojia na mawasiliano,
-Mgawanyiko
wa watu.
Mifumo
ya biashara,fedha,teknolojia na mawasiliano na hata mgawanyiko wa watu
vinamgusa kila mtu katika nyaja yeyote atakayokuwa na chini ya serikali yoyote
hivyo,kila mtu atalazimika kuufuata na haiwezekani kuukwepa.
Kwa
hiyo utandawazi ni matokeo ya kupanuka,kusambaa na kuimarika kwa biashara na
mahusiano ya kifedha ulimwenguni.
-Utandawazi
ni kama vile wakati wa babeli kw mfanano;kwa namna ambavyo dhambi inaendelea
kuenea na kuutafuna ulimwengu,wanadamu wakijaribu kutafuta suluhisho la
matatizo hayo bila kumshirikisha Mungu,Kwa kujaribu kurudisha ile nguvu,umoja
na mamani waliyoitumia hata wakamuasi Mungu,kwa kuifanya dunia nzima kuwa
kijiji,lugha moja,na usemi mmoja.
-Kumbuka
awali nlikuambia kuwa kusudi la Mungu kutuumba sisi ni kuusimika ufalme wake
hapa duniani,nasi tukitawala na kumiliki kwa niaba yake(koloni lake litawale),Yesu
kristo akiwa mfalme pekee.
-Yesu
kristo ni masiha chaguo la Mungu wa dunia nzima,na mpango huu wa kuufanya
ulimwengu kuwa kitu kimoja unamweka pembeni bila kumhusisha kama vile hana
umuhimu wowote ule.Alikufa msalabani kwa ajili ya ulimwengu mzima,na siku moja
ulimwengu utamshuhudia akishuka ulimwenguni kama mfalme,na kila ulimi utakiri
ya kuwa Yesu kristo ni bwana.
-Tayari
utandawazi umeshika hatamu,huku dunia nzima ikielekea kwenda kutawaliwa na mtu
mmoja,na tayari baadhi ya mataifa machache yanayotawala dunia yameanza
kujichuja,na mpaka sasa wamebakia kama sita au saba,na kwa mujibu wa manabii ni
lazima utafika wakati atabakia mmoja.Kwa maana hii ni wazi kuwa mwenendo wa
ulimwengu huu unamuandaa mfalme mwingine ambaye si Yesu,kuja kutawala.
Danieli
2:44 Na katika siku za wafalme hao
Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele,wala watu
wengine hawataachiwa enzi yake;bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na
kuziharibu,nao utasimama milele na milele.
Math
24.
Chanzo
cha matukio yote ni kurudi kwa mfalme wa kweli na wa haki(Yesu kristo) ambaye
atakuta wenyeji wa ulimwengu huu
wameshasimika ufalme mmoja unaotawala ulimwengu mzima,dunia ikiwa kama
kijiji,na ufalme huu ukiwa na matakwa yake binafsi kinyume na mapenzi ya Mungu.
Suluhu
ya Mungu juu ya uhasi huu uliopitiliza ni kuutikisa ufalme huo wa
wanadamu(ulimwengu mzima),kwa matukio mbali mbali tena ya kutisha kama
ilivyotabiriwa na manabii.
Danieli
12:1 “Katika wakati huo Mikaeli,
mtawala mkuu ambaye huwalinda watu wako,atainuka. Kutakuwako wakati wa taabu
ambao haujatokea tangu mwanzo wa mataifa hadi wakati huo. Lakini wakati huo,
watu wako, kila mmoja ambaye jina lake litakutwa limeandikwa kwenye kitabu,
ataokolewa.
Tukio
la awali kabisa la utandawazi(amalgamation) lilionekana wakati wa babeli(Mwanzo
11)Siasa ya ujamaa na dini moja vilitawala kwa nguvu,utaratibu wote wa
kuunganisha dunia nzima bila kujali wala kumshirikisha Mungu,wala maongozi ya
Mungu.
Wengi
tunamkumbuka mwanahistoria wa wakati huo Nimrod na jitihada nyingi alizozifanya
wakati huo,katika kueneza ibada za miungu.
Kwa
kuwa walikuwa kinyume na mpango wa Mungu ,Mungu aliamua kuugawa ulimwengu
katika lugha tofauti na mataifa mbalimbali,Ili kuivunja nguvu yao ya umoja
katika uasi.
Ulikuwa
wakati maalum wa kutokomeza uasi na uovu uliokithiri,na kutengeneza njia kwa
ajili ya mpango wake wa Masihi Yesu kristo,kurudi kuutawala ulimwengu na ndiyo
maana ikaitwa babeli(Mwanzo 11:9).
Jitihada
za sasa za kuunganisha ulimwengu bila Mungu zilitabiriwa na manabii ambao pia
wametabiri uharibifu wake kwa kuja kwa Yesu kristo kuithibitisha hukumu ya
msalaba.
Prophesies.
Tunaweza
kuyathibitisha haya kupitia mipasuko mbalimbali ya mataifa makkubwa
yaliyoungana na yenye nguvu,na namna
ambavyo kasi na shinikizo la mataifa kuungana inazidi kuwa kubwa.Mifano yake ni
kama vileumoja wa ulaya,Mahakama ya kimataifa,Sheria za umoja wa mataifa
zinazoondoa mamlaka ya sheria za ndanui za nchi mojamoja,Kubadili fikra za watu
kuwa moja,mfumo wa kushirikiana sarafu moja unazidi kushika hatamu,
By.Israel
Severe.
No comments:
Post a Comment