Sunday, January 24, 2016

Gazeti la Nipashe-Msuva amjibu Kiiza, Yanga ikitakata Dar



25th January 2016
Simon Msuva ndiye aliyefunga goli la kwanza la Yanga katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu waliposhinda 2-0 dhidi ya Coastal Unioni Septmba 13 na jana akamjibu Mganda Hamis Kiiza wa Simba kwa kufunga goli la kwanza la timu yake walipoichapa Friends Rangers mabao 3-0 katika mechi yao ya Kombe la FA kwenye Uwanja wa Taifa.

Kiiza ambaye pia alifunga goli la kwanza la Simba katika ligi ya Bara msimu huu waliposhinda 1-0 dhidi ya African Sports jijini Tanga Septemba 12, alitupia mara mbili wakati Wanamsimbazi walipoibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Burkinafaso mjini Morogoro juzi.

Ushindi wa jana umeipeleka Yanga raundi ya nne ya michuano hiyo ambayo bingwa wake ataiwakilisha Tanzania Bara katika michuano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika mwakani.

Msuva, Mchezaji Bora na Mfungaji Bora wa ligi ya Bara msimu ulioita, alimjibu Kiiza kwa kufungua karamu ya mabao ya timu yake alipotikisa nyavu kwa kichwa dakika ya tano baada ya kipenga cha kwanza akiunganisha mpira wa kona iliyopigwa na Issoufou Abubakar.Habari zaidi http://www.ippmedia.com/?l=88261

No comments:

Post a Comment

Ads 468x60px

Featured Posts