Sunday, January 24, 2016

Gazeti la Nipashe asubui hii-Vita ya madaraka ya Bunge yakolea.



25th January 2016

Yadaiwa chanzo kudhibiti aibu kama Richmond, Epa, Escow
Kasi iliyoonyeshwa na Bunge lililopita katika kuisimamia Serikali kiasi cha kumlazimu Rais Jakaya Kikwete, kufanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri zaidi ya mara nne, inatajwa kuwa chanzo cha kuibuka kwa vita inayoonekana wazi ya kutaka kudhibiti mhimili huo muhimu wa dola.

Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti jana, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya siasa walisema mkanganyiko ulioibuka kuhusiana na uteuzi wa kamati mbalimbali za chombo hicho ni ishara ya wazi kwamba kuna vita ya kutaka kudhibiti utendaji wa chombo hicho, ambayo mshiriki wake mkuu ni serikali ya awamu ya tano.

Wakieleza zaidi, baadhi ya wachambuzi hao wamedai kuwa mwenendo wa Bunge la 11, kuanzia mchakato wake wa kumpata Naibu Spika na hadi sasa katika uteuzi wa wajumbe wa kamati za Bunge, unaashiria kuwa serikali imepania kupunguza makali ya chombo hicho ambacho katika miaka kumi iliyopita kimejitahidi kwa kiasi kikubwa kutekeleza wajibu wake wa kuisimiamia serikali kiasi cha kuibua masuala kadhaa yaliyotikisa baraza la mawaziri, mfano ukiwa ni kashfa za Richmond, uchotwaji wa Sh. bilioni 133 za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) iliyokuwa Benki Kuu (BoT), Operesheni Tokomeza na pia uchotwaji wa mabilioni ya fedha kupitia Akaunti ya Tegeta Escrow iliyokuwa pia BoT.

Mwishoni mwa wiki, Spika wa Bunge, Job Ndugai,  alitangaza wajumbe wanaounda kamati mbalimbali za chombo hicho huku mjadala ukiibuka kuhusiana na uamuzi wa kutowarejesha baadhi ya wabunge walioitikisa serikali kutokana na kuibua kwao mambo kadhaa kupitia kamati walizokuwamo. Wabunge wengi waliokuwa maaarufu wamejikuta wakikosa nafasi katika kamati mbalimbali walizokuwapo awali ikiwamo nyeti ya Hesabu za Serikali na Mashirika ya Umma (PAC), na kisha wengi wao kuwekwa katika Kamati ya Huduma za Jamii.Kwa habari zaidi tembelea http://www.ippmedia.com/?l=88244

No comments:

Post a Comment

Ads 468x60px

Featured Posts