Wednesday, July 29, 2015

UHUSIANO KATI YA SHIRIKA LA BIMA,NA MTEJA WA BIMA.

Nikumegeeni kaufahamu kidogo tu ni kwamba,gari ikishauzwa na bima yake inakufa automatically.Bima ni mkataba kati ya kampuni ya bima,na mteja wa bima unaounganishwa na chombo chenyewe;yaani uhusiano wa kisheria kati ya mteja wa bima na kampuni ya bima.Kwa mantiki hiyo,mmiliki wa gari anapouza chombo maana yake amevunja uhusiano wake na shirika la bima na mnunuzi mpya atalazimika kisheria kuanzisha uhusiano mpya na shirika la bima,ikimaanisha kukata bima upya.Hii kwa kizungu inaitwa kanuni/principle of insurable interest.hakikisha unafanya hivyo ili kuepuka upotevu au hasara inayoweza kukupata kwa kutokujua.By Severe I.M.-Shirika la bima la taifa(NIC)

No comments:

Post a Comment

Ads 468x60px

Featured Posts