Friday, March 27, 2015

Mjasiriamali anayepingana na kushindwa maishani



Na Joyce Joliga,Mwananchi

Posted  Jumapili,Novemba2  2014  saa 11:47 AM
Songea. Ni mwanamama mwenye vipaji lukuki na ambaye kwa kauli yake anabainisha kuwa wanawake popote walipo wakikubali kushindwa ni lazima watashindwa tena vibaya sana, lakini wakiamua kupambana hakuna kushindwa.

Huyu si mwingine ni Jacline Msongozi ambaye ni Mama wa watoto wawili, kwake kushindwa siyo jambo rahisi, kwani pamoja na kufanikiwa katika biashara ya upikaji wa vyakula pia ni Mwanasiasa ambaye ana vyeo vingi zaidi katika Manispaa ya Songea.
Ameweza kupambana na ugumu wa maisha kwa kujiingiza katika biashara mbali mbali ili aweze kutimiza ndoto yake ya kuwa na Hoteli kubwa ya kitalii hapo baadaye.
Tayari diwani huyo wa Viti Maalumu kupitia CCM ameweza kutoa ajira kwa vijana 37 kupitia biashara hiyo ambayo imemsaidia kupata mafanikio. Kadhalika anajihusisha na ukulima katika mashamba ,ufugaji wa ng’ombe,mbuzi pamoja na samaki jambo ambalo limempa uzoefu na mafanikio

Kuanza biashara:
Mjasiriamali huyo anaeleza kuwa alianza rasmi biashara mwaka 1997 kwa kufungua saloon ya kike ambayo aliindesha bila mafanikio , baadaye ajiingiza katika biashara ya kuuza mitandao ya simu za TTCL, simu ,vocha na baada ya hapo akawa Wakala wa mitandao ya Tigo kwa wakati huo ikijulikana kama Buzz.

Anasema, kutokana na kiu kubwa ya mafanikio aliyokuwa nayo, aliamua kujikita katika biashara ya chakula, lakini alikutana na changamoto nyingi kusafiri mara kwa mara ,bidhaa zilikaa hadi kuharibika akaamua kwenda kufanya bishara ya kupika chakula kwenye sherehe.
“Naipenda sana biashara yangu ya vyakula kwani imenisaidia kupata mafanikio makubwa sana nimeweza kujenga nyumba bora ya kuishi eneo la Ruvuma, kununua usafiri pamoja na kupata mtaji wa kununua mifugo kwa ujumla najivunia sana biashara hii,”alisema Jacline.
Anaongeza kuwa, kutokana na umahiri wake wa mapishi amefanikiwa kupata tenda za zabuni katika

Kujiunga katika siasa:
Akizungumzia alivyojiunga na siasa anasema alianza kujihusisha na siasa mwaka 2000 akiwa mkereketwa wa (CCM, ambapo aliingia umoja wa wanawake ,wazazi “Namshukuru Mungu nimepata mafanikio makubwa katika siasa, mwaka 2007 nilianza kugombea nafasi mbalimbali za ndani ya chama katibu mwenezi, mjumbe mkutano mkuu taifa mwaka 2007.
Mjumbe Halimashauri kuu kupitia UWT 2007 mjumbe kamati ya siasa (W)mjumbe kamati ya maadili (w)2008 nilichaguliwa kuwa katibu wa Elimu malezi,uchumi jumuia ya wazazi (w)songea mjini 2012 nilichaguliwa kuwa mjumbe baraza kuu wazazi Taifa 2013 nimeteuliwa kuwa mjumbe bodi ya maji (SOWASA)
Anasema, kutokana na kuwa na biashara pamoja na kiongozi wa siasa anajipangia ratiba ya kufanya mambo yake kila asubuhi ,kabla ya kujishusisha na mambo ya siasa anaweka taratibu za biashara zake kwanza baada ya hapo anaendelea na na vikao vya siasa

Wito kwa wanawake:
Anawataka wanawake wasiogope kupambana na maisha wajikite kwenye shughuli za ufugaji kilimo na ujasiriamali hasa ufugaji samaki ambao hauna gharama, Wajikite kwenye kilimo cha
mazao ufuta,alizeti kwani mazao hayo yana soko kubwa tofauti na zao la mahindi yanaleta usumbufu kwenye soko
Wanawake watambue kuwa wao ni wazazi, hivyo wajifunze kuwapenda na kuwasaidia watoto wao kwa kuwalea kwa karibu na kujenga malezi ya watoto,ili kukabiliana na mmomonyoko wa maadili.

No comments:

Post a Comment

Ads 468x60px

Featured Posts