Imeandaliwa na Elizabeth Edward Mwananchi
Posted Jumapili,Agosti31 2014 saa 11:31 AM
Unapozungumzia watayarishaji wa
muziki wanaofanya vizuri kwa sasa barani Afrika lazima jina la Don Jazzy
litakuwa kwenye orodha hiyo.
Sifa hiyo inatokana na uwezo wa aina
yake alionao mtayarishaji huyu katika kucheza na ala za muziki sambamba na
teknolojia, hatua inayomfanya kutengeneza muziki mzuri.
Uwezo huo ndiyo ulimshawishi Kanye
West kumuajiri kama mtayarishaji kwenye lebo yake GOOD Music, huo ndiyo ukawa
mwanzo wa nyota huyu kutambulika kimataifa.
Akiwa katika lebo hiyo aliweza
kutengeneza zaidi ya nyimbo 100 za wanamuziki kadha wa kadha wa kimataifa.
Kama ilivyo kwa watu wengine
waliofanikiwa, Don Jazzy hakufikia mafanikio hayo kwa urahisi licha ya kuwa na
kipaji cha uimbaji na upigaji ngoma tangu akiwa mdogo.
Kipaji hicho ndicho
kilichomsababishia mjomba wake aliyekuwa akiishi mjini London kumualika kwa
ajili ya kupiga ngoma kanisani.
Akiwa na umri wa miaka 18 Don Jazzy
aliwasili nchini Uingereza na kuanza kupiga ngoma kanisani kazi ambayo pamoja
na kumtambulisha haikuweza kumpatia kiasi kikubwa cha fedha.
Hali hiyo ilimsukuma kutafuta
shughuli nyingine ya kumuingizia kipato ndipo alipofanikiwa kupata kazi ya
ulinzi katika kampuni binafsi.
Muda wote huo Jazzy alikuwa
akijifunza kucheza na ala mbalimbali za muziki ikiwamo gitaa la bass kichwani
akijiwekea malengo kuwa mtayarishaji siku moja.
Lengo hilo lilitimia miaka michache
baadaye aliporudi nyumbani Nigeria akiwa ameweza kwenye utayarishaji na
kufanikiwa kufungua studio yake.
Mwaka 2004 aliamua kuunganisha nguvu
na rafiki yake wa karibu D’Banj na kuanzisha lebo ya Mo’ Hits Records
iliyojizolea umaarufu mkubwa barani Afrika hasa baada ya kurekodi albamu ya No
Long Thing.
Wawili hao walidumu pamoja kwa muda
wa miaka nane kabla ya Mavin kujitoa na kuanzisha lebo yake ya Mavin Lebo hiyo
ilidumu kwa takribani miaka saba kabla ya wawili hao kutengana na Don Jazzy
kuanzisha lebo ya Mavin Records huku D’Banj akibaki na Mo’Hits Records.
Akiwa mkurugenzi mkuu wa Mavin Records ameweza kuifikisha lebo hiyo kwenye
mafanikio makubwa na kuwa miongoni mwa lebo zinazofanya kazi nzuri kwa sasa
nchini Nigeria na Afrika kwa ujumla.Kwa hivi sasa Don Jazzy ni miongoni mwa watayarishaji ambao wanakimbiliwa na wanamuziki wenye majina makubwa barani Afrika kutokana na namna anavyomudu kutengeneza muziki bora.
Toleo jipya la jarida la Forbes lilimtaja Don Jazzy kama miongoni mwa mastaa wenye nguvu kubwa barani Afrika kwa kushika nafasi ya 36 kati ya magwiji 100.
No comments:
Post a Comment